Machi 4 watatangazwa watakatifu watatu wa kanisa - | vatican news

Machi 4 watatangazwa watakatifu watatu wa kanisa - | vatican news

Play all audios:


Tarehe 4 Machi Papa Fancisko ataongoza Masifu ya Tatu na kufanya Mkutano wa kawaida na makardinali kwa ajili ya kuwatangaza watakatifu watatu:mwenyeheri Titus Brandsma,Kuhani mfiadini na wa


Shirika la Wakarmeli;Mwenyeheri Maria Rivier,Mwanzilishi wa Shirika la Watawa wa Kike wa Kumwakilisha Maria;Mwenyeheri Maria wa Yesu,Mwanzilishi wa Shirika wa watawa wa kike wakapuchini NA


ANGELLA RWEZAULA – VATICAN. Ofisi ya maadhimisho ya liturujia za kipapa imetoa taarifa kuwa tarehe 4 Machi  2022 utafanyika Mkutano (Consistory)  wa kawaida wa umma na makardinali kwa ajili


ya kupitisha baadhi ya watakaotangazwa watakatifu saa 4.30 katika Ukumbi wa Mkutano kwenye Jumba la Kitume Vatican. Papa Fancisko katika siku hiyo ataongoza Masifu ya Tatu na Mkutano huo wa


kawaida wa umma na makardinali kwa ajili ya kuwatangaza watakatifu watatu wafuatao: mwenyeheri Titus Brandsma, Kuhani mfiadini na mwenye nadhiri wa Shirika la Wakarmeli; Mwenyeheri Maria


Rivier, Mwanzilishi wa Shirika la Watawa wa Kike wa Kumwakilisha Maria; Mwenyeheri Maria wa Yesu (zamani aliitwa Carolina Santocanale), Mwanzilishi wa Shirika wa watawa wa kike waKapuchini


wa Moyo safi wa Lourdes. Kwa maana hiyo Makardinali wanaoishi Roma na walioko Roma katika Siku hiyo ya Mkutano, wanaomba kukutana saa 4.00 kamili siku hiyo kwenye Ukumbi wa Mkutano wa Jumba


la Kitume wakiwa na mavazi tayari ya maadhimisho.