Kard.Tagle,Injili ya Uumbaji:Utume ni zawadi kwa Kanisa lote

Play all audios:

Kardinali Luis Antonio Tagle, Kardinali Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, wakati anazungumza kweny radio Vatican juu ya utume wa kimisionari uliokabidhiwa kwa wahudumu wa Laudato si'
wa Harakati Katoliki Ulimwenguni kwa ajili ya Tabianchi na wahudumu wengine wa kichungaji, vijana, watu wenye mapenzi mema amesema: “Katika utume wa Kanisa kila mbatizwa amepokea Roho
Mtakatifu zawadi ambayo inapaswa kuendelezwa kwa kushiriki katika utume wenyewe na kuhusu suala la Laudato si’, ni utunzaji wa nyumba yetu ya pamoja”.
Alithibitisha hayo mara tu baada ya Papa Franciko Jumapili wakati wa Sala ya Malkia wa Mbingu alikuwa amezungmzia juu ya utume wa kueneza Injili ya Kazi ya Uumbaji na kuanza utunzaji wa
mazingira nyumba yetu ya pamoja. Katika mtazamo wa kumbukumbu ya miaka sita ya Waraka wa Papa Francisko juu ya utunzaji wa nyumba ya pamoja, uliochapishwa mnamo tarehe 24 Mei 2015, na katika
Wiki ya Laudato Si, ambayo imehitimisha mwaka maalum uliotangazwa na Papa kutafakari na kujikita kwenye matendo ya dhati ya waraka huo, vile vile Kardinali Tagle ameongoza mkutano wa
maombi katika Shirika la Watawa Wafranciskani (OFM) Roma.
Katika siku ya Pentekoste, siku ya kushuka kwa Roho Mtakatifu ambaye alitoa mwanzo wa utume wa Kanisa au kuzaliwa kwa Kanisa, Kardinali Tagle amesema Pentekoste ni kuonesha kuwa Kristo
aliyefufuka anandelea kubaki nasi. Wito wa Kardinali ni kuwa shuhuda wa ukweli wa ulimwengu, hata baada ya wakati huu ambao ni wa mgogoro uliokumbwa na janga la virusi vya covid-19. Kufanya
uzoefu wa Kristo ni kuelewa kuwa Yesu anatusindikiza kama alivyofanya kwa wafuasi wake. Utume kama wito kwa ajili ya maisha yote ni hata kusindikiza wengine na kubaki kufanya hatua moja
moja na si kurudi nyumba
Kwa upande mwingine, ameunga mkono wa maneno ya Padre Augusto Zampini, katibu msaidizi wa Kitengo cha Baraza la Maendeleo Fungamani ya Binadamu na mjumbe wa mwelekeo wa Tume ya Vaticani
Covid-19. Padre Zampini yeye alisema Injili ya Uumbaji imeunganishwa na Kanisa linalotoka nje, kwa maana ni Kanisa ambalo hutunza nyumba yetu ya pamoja na ya wengine kila mahali kwenye
sayari hii. Huu ndio uzuri wa maana ya kimisionari wa kuleta ujumbe wa Injili na Laudato si ', wa utunzaji wa nyumba yetu ya pamoja na wengine, katika kila sehemu ya sayari, katika kila
sekta ya jamii, pia kukumbuka jinsi Papa ambavyo anaomba mabadiliko makubwa ya uchumi iliougua, kwa sababu husababisha ukosefu wa usawa, magonjwa ya kijamii, mizozo na uharibifu wa kazi ya
uumbaji, ameongeza Padre Zampini.
Kutoka Rio de Janerio, Nairobi, Washington, Roma, Assisi limefika jibu la ndio la utume wa kimisionari, kuchukua jukumu la Wahuishaji ili kusikiliza kilio cha Dunia na maskini, wale
waathiriwa wa shida na mateso katika nchi ya India kama, ilivyo Brazil ambapo Padre Michael Perry, Mkuu wa Shirika la Ndugu wadogo Wafransiskani ( OFM) alitaka kukumbusha katika hotuba yake
kwamba wao ni watu ambao kiukweli wanabeba Msalaba, ambao lazima kuwapa fursa, kwa mtazamo wa udugu na utume. Jitihada ya mwisho ilikuwa kuangazia ukarimu, upendo na unyenyekevu kama
alivyosisitiza Kardinali Tagle kwamba ni kuwasha mshumaa na washiriki ile nuru katika maisha ya Kanisa na ulimwengu. Matashi mema kwa ajili ya upyaisho wa jitihada zaidi kwa waamini
ilitoka katika Bustani ya Botaniki ya Roma, ambapo Padre Joshtrom Isaac Kureethadam, Mratibu wa Sekta ya Ekolojia na Uumbaji ya Baraza la Kipapa la Maendeleo Fungamani ya binadamu alikuwa
ameadhimisha Misa Takatifu kwa kumbukumbu ya miaka sita tangu kuchapishwa kwa Waraka wa Laudato si '. “Tumepokea bustani, hatuwezi kuiacha kama jangwa kwa vijana wetu na kwa maana hiyo
amesisitizai ju ya Waraka huo wa Papa wa kulinda viumbe vyote na utunzji wa mazingira nyumba yetu ya Pamoja.