Chama cha gnocchi ni wajumbe wa huruma kwa wadhaifu! - | vatican news

Play all audios:

Msichoke kamwe kuhudumia walio wa mwisho katika mpango wa wagonjwa na walemavu.Ndiyo ulikuwa moyo wa hotuba ya Baba Mtakatifu Francisko kwa wajumbe wawakilishi wa Chama cha Mwenyeheri Padre
Don Gnocchi,aliokutana nao mjini Vatican 31 Oktoba 2019.Chama hiki kimepeleka mbele urithi wake kama talanta muhimu katika kazi ya utume na uaminifu wa Injili. NA SR. ANGELA RWEZAUL- VATICAN
Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Chama cha Padre Carlo Gnochi kinachojikita katika hali halisi ya kutoa msaada wa kutunza na kijamii. Katika salam anakumbuka mwanzo wa chama hiki
ambacho kimebubujika kutoka katika moyo wa padre wa kiambrosi. Aidha amakumbuka katika mahubiri wakati wa kutangazwa kwake kuwa Mwenyeheri, Katika misa iliyofanyika huko Milano miaka 10
iliyopita, Kardinali Tetamanzi alimtaja Padr ehuyo kama mwana shauku wa kutafuta Mungu na jasiri wa kutafuta mtu na maisha yake yote yalijikita katika kutafuta uso wa Kristo ambao ambao umo
ndani ya uso wa kila binadamu. KWA HAKIKA BABA MTAKATIFU AMESEMA YEYE NI MTUME WA HURUMA na upendo, mtumishi kwa namna ya kishujaa kwa watoto, vijana, masikini na wanaoteseka, tangu wakati
wake wa kuanza huduma yake ya kikuhani akiwa na ari ya kufundisha. Aidha amesema jinis alivyojikita katika usimamizi wa Kanisa la kijeshi ambaye alitambua ukatili wa vita ya Pili ya Dunia
mapema akiwa mapakani wa Ugiriki na Albania, baadaye,Tridentina na janga la kikundi cha kijeshi kutoka Urusi. Katika harakati za miaka mingi, chama hiki kimepeleka mbele urithi wake kama
vile talanta muhimu na kuzidi maradufu katika kazi yake ya utume na uaminifu wa Injili. Baba Mtakatifu Francisko anawapongeza kwa hilo, wakurugenzi na wahusika wa vituo mbalimbali
madaktari, wahudumu, watu wa kujitolea na marafiki. AIDHA WAO WALIKUWA PAMOJA NA WAGONJWA WAO, AMBAO WANATUNZWA KATIKA VITUO mbalimbali na familia zao ili kuthibitisha jitihada zao za
kusaidia jirani katika mateso ya watu walio wadhaifu zaidi, kwa mtindo kama wa msamaria mwema na kwa njia ya mfano wa Mwanzilishi wake. Amewasihi sana wasichoke kuhudumia watu walio wa
mwisho mbele ya magonjwa magumu na ulemavu, pamoja na tiba na manedeleo ya kifundi kwa ajili ya mwili, wajitoa wote kwa matumaini katika vituo vyao na majengo yao wakiwa ni madaktari wa
kiroho kwa maana ya kufariji kwa huruma ya Mungu. MADA MUHIMU NA YENYE THAMANI YA KITAALUMA YA AFYA NA KILA HUDUMA KWA MDUGU MGONJWA INAJIONESHA DHAHIRI katika uwezo wa kujikita kutibu kwa
mambo mawili mawili ambayo ni UJUZi na HURUMA. Ujuzi ni kufanya maandalizi yao na uzoefu wa kujisasisha: na yote hayo ni sasabu ya nguvu katika utoaji wa huduma kwa jirani anayeteseka.
Baba Mtakatifu Francisko anawatia moyo waendelee na safari yao katika jitihada ya kukuza ubinadamu na ambao ni mchango mkubwa unaohitajika katika utume wa kuijilisha katika Kanisa.
Kiukweli anasema tangazo la Injili ni zaidi sna aminifu kutokana na upendo wa dhati ambao mfuasi wa Yesu anajikita nao kushuhudia kwa imani Yeye. Ushuhuda wa kibinadamu na kikristo wa
Mwenyeheri Padre Carlo Gnocchi, unayo tabia ya upendo kwa ajili ya watu walio wadhaifu,hivyo uwaongoze daima uchaguzi wao na shughuli zao. Bwana awawezeshe daima na kila mahali kuwa wajumbe
wa huruma yake na faraja. Anawasindikiza kwa sala zake na kuwabariki.